Kama Nisingeokolewa na Mungu
Kama mimi nisingeokolewa na Mungu,
ningekuwa bado nazurura ulimwenguni humu,
nikipambana kwa bidii na maumivu katika
dhambi; kila siku huwa ya taabu isiyo na tarajio.
Kama nisingeokolewa na Mungu, bado
ningekuwa nimepondwa chini ya miguu ya shetani,
kama nimenaswa katika dhambi na starehe
zake, bila kujua maisha yangu yangekuwaje.
Kama nisingeokolewa na Mungu, nisingekuwa
na baraka zangu leo,
wala kujua kwa nini sisi tuendelee kuishi
ama maana ya maisha yetu.

