Sio kila kitu katika Biblia ni rekodi ya
maneno aliyoyasema Mungu. Kimsingi Biblia inaandika hatua mbili za awali za
kazi ya Mungu, ambapo sehemu moja ni rekodi ya utabiri wa kale wa manabii, na
sehemu nyingine ni uzoefu na maarifa yaliyoandikwa na watu waliotumiwa na Mungu
katika enzi zote. Uzoefu wa kibinadamu umetiwa doa na maoni na maarifa ya
kibinadamu, kitu ambacho hakiepukiki. Katika vitabu vingi vya Biblia kuna dhana
nyingi za kibinadamu, upendelevu wa kibinadamu, na ufasiri wa ajabu wa
kibinadamu. Ni kweli, maneno mengi ni matokeo ya kupatiwa nuru na kuangaziwa na
Roho Mtakatifu, na ni tafsiri sahihi—lakini haiwezi kusemwa kuwa ni
udhihirishaji sahahi kabisa wa ukweli. Maoni yao juu ya vitu fulani si chochote
zaidi ya maarifa uzoefu binafsi, au kupatiwa nuru na Roho Mtakatifu. Utabiri wa
manabii ulikuwa umetolewa na Mungu mwenyewe: Unabii wa Isaya, Danieli, Ezra,
Yeremia, na Ezekieli, ulitoka moja kwa moja kwa Roho Mtakatifu, watu hawa
walikuwa ni waonaji maono, walipokea Roho ya Unabii, wote walikuwa ni manabii
wa Agano la Kale. Wakati wa Enzi ya Sheria watu hawa, ambao walikuwa wamepokea
ufunuo wa Yehova, walizungumza unabii mwingi, ambao ulisemwa na Yehova moja kwa
moja. Na kwa nini Yehova alifanya kazi ndani yao? Kwa sababu watu wa Israeli
walikuwa ni wateule wa Mungu: Kazi ya manabii ilipaswa kufanyika miongoni mwao,
na walikuwa wamefuzu kupokea maono hayo. Kimsingi, wao wenyewe hawakuelewa
ufunuo wa Mungu kwao. Roho Mtakatifu Alizungumza maneno hayo kupitia vinywa
vyao ili watu wa baadaye waweze kuelewa mambo hayo, na kuona kwamba ni kweli
ilikuwa ni kazi ya Roho wa Mungu, ya Roho Mtakatifu, na haikutoka kwa
mwanadamu, na kuweza kuwathibitishia kazi ya Roho Mtakatifu. Wakati wa Enzi ya
Neema, Yesu Mwenyewe Alifanya kazi hii yote badala yao, na hivyo watu
hawakuzungumza tena unabii. Kwa hivyo Yesu alikuwa nabii?
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu
Kwa nini unamwamini Mungu ? Watu wengi wanafadhaishwa na swali hili. Siku zote wana mitazamo tofauti kuhusu Mungu wa vitendo na Mungu wa...
-
Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho Mungu ndiye Mwanzo, Mungu ndiye Mwanzo, Mungu ndiye Mwanzo, na tena Mwisho, na tena Mwisho, na tena Mw...
-
Tatizo la kawaida lililo miongoni mwa binadamu wote ni kwamba wao huuelewa ukweli lakini hawawezi kuuweka katika matendo. Sababu moja ...
-
Biblia pia huitwa Agano la Kale na Agano Jipya. Je, wajua “agano” linarejelea nini? “Agano” katika “Agano Jipya” linatokana na makubalia...
